Maajabu ya mapacha walioungana
Hawakuweza kujulikana mapema hadi walipofikia umri wa kwenda shule. Hapo ndipo vyombo vya habari vilipotangaza kwa nguvu habari ya watoto wao, baada ya Mwananchi kuiibua. Miaka 21 iliyopita, familia ya Alfred Mwakikuti na Naomi Mshumbusi ilijaaliwa kupata watoto pacha, Maria na Consolata. Lakini hawakuwa pacha wa kawaida; walikuwa wameungana na hakukuwapo na uwezekano wa kuwatenganisha. Hawakuweza kujulikana mapema hadi walipofikia umri wa kwenda shule. Hapo ndipo vyombo vya habari vilipotangaza kwa nguvu habari ya watoto wao, baada ya Mwananchi kuiibua. Mwaka 2010 walimaliza elimu ya msingi na 2014 elimu ya sekondari na mwaka huu wamemaliza elimu ya juu ya sekondari. Wakati wote huo gazeti hili limekuwa nao pamoja katika kila hatua na sasa linakuletea habari mfululizo za maisha yao kuanzia leo. Mwandishi wetu, Tumaini Msowoya anaongea nao kwa kirefu kuhusu maisha yao, changamoto, mafanikio na matamanio yao. Sasa endelea Kilolo. Acheni Mungu aitwe Mungu kw...